Unyanyasaji Unaotumia Teknolojia

Je, Unyanyasaji wa Kutumia Teknolojia ni nini?

Unyanyasaji wa kutumia teknolojia hutokea wakati mtu anapotumia teknolojia ya kidijitali kumdhibiti, kumlazimisha, au kumdhara mtu mwingine. Mara kwa mara aina hii ya unyanyasaji ni sehemu ya ukatili wa nyumbani, familia, na kingono.

Nchini Australia, baadhi ya aina za unyanyasaji wa kutumia teknolojia, kama vile kushiriki picha za siri bila ruhusa au kutumia programu ya ufuatiliaji ili kumpeleleza mtu, ni kinyume na sheria. Unaweza kuripoti matendo hayo kwa polisi na kwa eSafety Commissioner.

Unyanyasaji wa kutumia teknolojia ni suala kubwa kwa sababu huingilia faragha yako na unaweza kusababisha madhara makubwa. Kuuelewa aina hii ya unyanyasaji ni muhimu ili kujilinda mwenyewe na wengine. Kwa kujua haki zako na kutafuta usaidizi, unaweza kupata udhibiti tena na kuhakikisha usalama wako.

Nchini Australia, ni muhimu kukumbuka:

  • Una haki ya kutumia teknolojia bila kuogopa unyanyasaji.
  • Unyanyasaji wa kutumia teknolojia kamwe siyo kosa lako.
  • Msaada unapatikana, na hauko peke yako.

Aina za Unyanyasaji wa Kutumia Teknolojia

Unyanyasaji wa kutumia teknolojia unaweza kuwa wa aina nyingi. Hapa chini ni mifano:

  • Kudhibiti Nenosiri za WiFi: Kukuzuia kutumia mtandao ili kukutenga.
  • Kuwasiliana Nawe Kila Mara: Kupiga simu au kutuma ujumbe mara kwa mara ili kujua upo wapi na unachofanya.
  • Kufuatilia Shughuli za Mtandaoni: Kuangalia mawasiliano yako ya mtandao wa kijamii, ujumbe wa maandishi, au matumizi ya mtandao.
  • Kuzuia Matumizi ya Kifaa: Kukosa kukuruhusu kuwa na simu au kompyuta, au kuongea na marafiki na wanafamilia mtandaoni.
  • Kushiriki Picha za Siri Bila Idhini: Kuweka mtandaoni au kutuma picha zako za siri bila ruhusa yako.
  • Kumtia Mtu Aibu ya Kitamaduni au Kidini: Kushiriki picha zinazowakilisha vibaya mazoea yako ya kitamaduni au kidini bila idhini yako.
  • Kupeleleza na Kufuatilia: Kutumia programu au vifaa ili kufuatilia mahali uliko au shughuli bila ufahamu wako.

Kujiweka Salama

Ikiwa wewe au mtu unayemfahamu anapata unyanyasaji wa kutumia teknolojia, hapa chini ni vidokezo vya kukusaidia kukaa salama:

  • Tumia Kifaa cha Salama: Ikiwa unafikiri kuwa kifaa chako kinafuatiliwa, tumia kompyuta au simu ambayo mnyanyasaji hawezi kutumia, kama moja katika maktaba ya umma.
  • Futa Historia ya Kivinjari: Ondoa historia yako ya kivinjari mara kwa mara kwenye vivinjari kama vile Google Chrome, Safari, na Microsoft Edge.
  • Badilisha Manenosiri: Badilisha manenosiri na usitumie hayo kwenye vifaa ambavyo unafiriki vinafuatiliwa.
  • Tumia Vitufe vya Kutoka Haraka: Kwenye tovuti zingine, kuna vitufe vya kutoka haraka kuondoka tovuti kwa haraka. Kumbuka, baadhi ya tovuti bado zinaweza kuonekana kwenye historia yako ya kivinjari.
  • Tumia Hali ya Siri: Vinjari katika hali fiche au ya siri ili kurasa zako za tovuti zisirekodiwe.
  • Tafuta Vifaa vya Kufuatilia: Tafuta vifaa vya kufuatilia kama vile Vitambulisho vya Hewani (AirTags) katika mali zako na zima ufuatiliaji wa eneo kwenye simu yako au kompyuta kibao.

Kukusanya Ushahidi

Ikiwa ni salama, kukusanya ushahidi wa unyanyasaji kunaweza kusaidia chunguzi za kisheria. Kwa mfano, piga picha za skrini za jumbe za matusi na zihifadhi kwenye kifaa cha salama. Mtoa huduma za ukatili wa nyumbani, familia au kingono, polisi, au mwanasheria anaweza kukushauri kuhusu aina gani ya ushahidi ambao ni muhimu zaidi kwa kesi yako.

Kupata Msaada

Kabla ya kutafuta msaada, fahamu kuwa hii inaweza kuwa hali ya hatari kwa sababu unyanyasaji huenda ukawa mbaya zaidi. Huduma za ukatili wa nyumbani, familia au kingono inaweza kukusaidia kupanga mpango wa usalama.

eSafety Commissioner ametengeneza nyenzo katika lugha yako kuwasaidia watu wanaopitia unyanyasaji wa kutumia teknolojia.

WESNET pia ina mfululizo wa nyenzo (Kiingereza-tu) kuhusu usalama na faragha ya wanawake.