Ukatili wa Kingono

Je, Ukatili wa Kingono ni nini?

Ukatili wa kingono ni tendo lolote la kingono, kama vile kugusa, kubusu, kusugua, au kujamiana, ambako kunatokea bila idhini. Hii inamaanisha kwa mwathirika hakukubali kufanya hiyo na alilazimishwa, alidanganywa, au kuendeshwa kufanya. Haijali kama tendo lilikamilishwa au lilijaribiwa tu.

Idhini ya kingono ni wakati watu wawili au zaidi wanakubali kujihusisha na tendo la ngono. Idhini lazima iwe ya huru, ya hiari, kufahamishwa, na yenye shauku. Kila mtu anayehusika lazima atake kwa ukweli katika kushiriki.

  • Kubadilisha Idhini: Unaweza kubadilisha mawazo yako wakati wowote wakati wa tendo la ngono. Ni muhimu kuomba kupata idhini wakati wote wa tendo.
  • Wakati Idhini Haiwezekani: Mtu ambaye amepoteza ufahamu, amelala, amelewa, au ana umri chini ya umri wa idhini (kuwa na umri chini ya miaka 16 au 17, kutegemea jimbo au wilaya) hawezi kutoa idhini.

Mashambulio ya kingono ni kinyume na sheria nchini:

  • Una haki ya kuwa salama na kuheshimwa.
  • Ukatili wa kingono kamwe siyo kosa lako.
  • Msaada unapatikana, na hauko peke yako.

Je, Nani Anaweza Kuwa Mnyanyasaji?

Mnyanyasaji anaweza kuwa mtu unayemfahamu au mgeni, kama vile:

  • Wapenzi, au wanandoa
  • Wapenzi wa zamani, au wanandoa wa zamani
  • Watunzaji, walezi, au wanafamilia
  • Rafiki au wenzako wa kazi
  • Wapenzi wa ngono (wa muda usiodumu au muda mrefu)
  • Waalimu, maprofesa, au makocha
  • Jamaa

Aina za Ukatili wa Kingono

Ukatili wa kingono unakuwa na aina nyingi, ukiwa ni pamoja na:

  • Shambulio la ngono
  • Unyanyasaji wa kingono
  • Ubakaji
  • Usumbufu wa ngono wa mara kwa mara
  • Stealthing (yaani kuondoa kondomu bila idhini)
  • Mfichuo wa kingono usiohitajika
  • Maoni au vicheshi vya ngono visivyohitajika
  • Kushirikisha picha ya kwako bila idhini
  • Mawasiliano ya kimwili yasiyohitajika (k.m., kugusa, kubusu, kusugua)
  • Kunyemelea
  • Mawasiliano wa kingono yasiyotakiwa (maneno, sanamu, mtandao wa kijamii)
  • Uangalizi wa siri (Voyeurism) (kumwangalia mtu bila idhini yake)
  • Unyanyasaji wa kingono wa mtoto
  • Unyonyaji na usafirishaji wa kingono
  • Spiking (kuweka dawa au alkoholi kwenye kinywaji cha mtu bila yeye kujua)

Athari ya Ukatili wa Kingono

Wengi wenye waliookoka kutoka kwenye  ukatili wa kingono wanahisi aibu, hatia au hofu jinsi wengine watakavyoitikia. Mara kwa mara hiyo inawazuia kuripoti unyanyasaji au kutafuta usaidizi.

Ikiwa umewahi kupitia aina yoyote ya ukatili wa kingono, kumbuka sio kosa lako. Ilichotokea kwako sio kwa sababu ya ulichovaa, ulikuwa nani, au ulichofanya. Ukatili wa kingono unaweza kutokea kwa mtu yeyote.

Kupata Msaada

Ikiwa wewe au mtu unayemfahamu anapitia ukatili wa kingono, polisi au mtoa huduma wa ukatili wa nyumbani, familia, au kingono anaweza kukusaidia.

1800RESPECT: Piga simu kwa 1800 737 732 kwa msaada na ushauri wa siri.

Unaweza kuwasiliana na Support for Trafficked People Program kwa 03 9345 1800 au kwa national_STPP@redcross.org.au

Unaweza kuwasiliana na Australian Federal Police kwa 131 237 au nenda kwa tovuti ya AFP.

Huduma za Msaada wa Kisheria: Hutoa ushauri wa kisheria na msaada. Wanaweza kueleza haki zako na kukusaidia na masuala ya kisheria. Unaweza kuwasiliana na msaada wa kisheria katika jimbo lako au wilaya yako kwa hapa.

Serikali ya Australia pia ina nyenzo muhimu kuhusu idhini ya kingono katika lugha yako.

Kwa habari zaidi na usaidizi, tembelea Ukurasa wetu wa Huduma za Usaidizi.